Hakika UKAWA hawana budi kuendelea kuikosoa serikali ya Raisi John Pombe Magufuli kwani ndio kazi yao itakuwa kitu cha ajabu kwa chama cha upinzani kushabikia au kuridhika na mwenendo wa serikali kwani kazi yao kama chama cha upinzani itakuwa haina maaana.Kwa kufanya hivyo itaifanya serikali iliyo madaraki isibweteke ni vyema kuendelea kufanya hivyo ili serikali iweze kutambua mapungufu na kufanya marekebisho adri iwezekanavyo.Lakini wananchi tunapaswa kuwa makini katika kuchambua yapi mazuri kwani wanasiasa ni kama vinyonga leo kijani kesho blue.
Pages - Menu
▼
Thursday, May 12, 2016
Monday, May 9, 2016
HUJUMA HIZI SI ZA KUZIACHIA HATA KIDOGO
Wananchi wa Tanzania kwa takribani mwezi mzima wamepata taabu kubwa baada ya sukari kuadimika.Hii imekuja baada matamko ya serikali baada ya kutoa bei elekezi na kusitisha vibali vya uwagizaji bidhaa hii.Baadala ya kutafuta njia mbadala na zilizosahihi wafanya biashara wakaficha sukari wakidhani serikali ingerudi nyuma.Kibao kimewageukia na njama zao potofu hakika rai yangu serikali isimame imara na isirudi nyuma kwa hili,kuteseka huku ni kwa muda wananchi wa hali ya chini ndio waliokuwa na taabika siku zote natumai mipango ya serikali ikikaa vizuri kila mtu atafurahi na wale wanaopinga hatua hizi watakuja kubadilika tuu,mabadiliko yoyote si rahisi kukubalika mapema hivyo tunabudi ya kuyakubali na matunda yataonekana baadaye.
TODAY'S MESSAGE
The best way to motivate yourself is to stop stressing about what'll happen when things go wrong and start thinking about how awesome life will be when they go right.