Tuesday, September 29, 2015

FAHAMU UGONJWA WA BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA NA NAMNA YA KUEPUKA NA UGONJWA HUU

NA JAMIIMOJABLOG)

WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba

JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!
~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.

~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles
~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50


AINA ZA BAWASIRI

~Kuna Aina mbili za bawasiri

(A) BAWASIRI YA NDANI
~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili
~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa
~Aina hii imegawanyika katika madaraja manne
(1)DARAJA LA KWANZA ~Hii ni bawasiri ambayo haitoki mahali pale panapohusika
(2)DARAJA LA PILI ~hii hutokea wakati wa haja na kurudi yenyewe ndani baada ya kujisaidia.
(3)DARAJA LA TATU :hii hutokea wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kurudisha ndani yeye mwenywe.
(4)DARAJA LA NNE :hii ni bawasiri inayotoka na huwa ngumu kurudi

(B)BAWASIRI YA NNJE
~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS


CHANZO CHA TATIZO

~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni ÷
��KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE
��KUHARISHA KWA MUDA MREFU
��TATIZO LA KUTOPATA CHOO
��MATATIZO YA UMRI
��KUKAA KITAKO KWA MUDA MREFU
��UZITO KUPITA KIASI
��MATUMIZI YA VYOO VYA KUKAA KWA MUDA MREFU
DALILI ZA BAWASIRI
��Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
��kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia
��kutokea uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
��kujitokeza kwa kinyama katika eneo la tundu Hilo
��kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana


MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI

~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia hivyo tiba nzuri ni kutumia dawa na anion chip kubandika mahali penye tatizo na kuondoa tatizo Hilo

~Pamoja na hayo bawasiri ni ugonjwa unaoweza kuepukika kwa kuzingatia
��KULA MBOGAMBOGA ZA MAJANI, MATUNDA, NA NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
��KUNYWA MAJI MENGI ANGALAU GRASS 6/12 Kwa siku
��EPUKA KUKAA CHOONI KWA MUDA MREFU


MADHARA YA TATIZO LA BAWASIRI

��kupata upungufu wa damu (anemia)
��Kupata tatizo la kutokuweza kuhimil choo
��hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake
��kuathirika kisaikolojia
��kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali

WASILIANA KWA 0717035770 AU 0753692612.

3 comments:

  1. asante blogger nimejifunza kitu kikubwa

    ReplyDelete
  2. Nashukuru kwa somo hili ila naomba kuuliza kua mgonjwa mwenye bawasiri ya mda mref akitumia dawa anapona?

    ReplyDelete
  3. Nashukuru kwa elimu hii ila naomba kuuliza kua mgonjwa wa bawasiri ya mda mref akitumia dawa anapona

    ReplyDelete