Tuesday, January 26, 2016

JE WAJUA ADEBAYOR KALA SHAVU CRYSTAL PLACE

Emmanuel Adebayor raia wa Togo hatimaye amepata timu tena baada ya kukaa kwa kipindi kirefu maana ya kuachana na Tottenham.Sasa ni mali ya Crystal Palace.Hii ni baada ya Alan Pardew (Kocha)kudhibitisha hilo kuwa anamuhitaji Emma katika timu hiyo.

Emmanuel Adebayor

Sunday, January 24, 2016

ARSENAL KURUDI KILELENI LEO DHIDI YA CHELSEA

Asernal inaweza kurudi kileleni itakapo kutana na Chelsea kwenye dimba la Emirates.Arsenal ambayo inatabiriwa kuwa inaweza kubeba kombe msimu huu baada ya kulikosa kwa zaidi ya miaka 10.Mechi inatarajiwa kuanza saa moja kwa majira ya Afrika Mashariki.

kTokeo la picha la chelsea vs arseanl logoKikosi cha Arsenal-(P.Cech,P Mate,L KoScielny,N Monreal,H Berlin,M Ozil,A Ramsey,A Sanchez,M Flamini,J Campell,O Giroud

Chelsea:T Courtois,B Ivanovic,K Zouma,J Terry,C Azpilicueta,C Febregas,J Obi,P Rodriguez,N Matic,Willian,D Costa.

Saturday, January 23, 2016

MAN U CHALII,LIVERPOOL BALAA,LEICESTER KILELENI TENA

Man united imefungwa goli moja na Southamphton,Liverpool imeipiga Norwich City 5-4 katika mechi tamu Lallan ndio alikuwa kinara baada ya kuifungia goli la tano.Leicester imerudi kileleni baada ya kuifinguka Stoke City 3-0.Watford imeifunga Newscastle 2-1.Tottenham imeifunga Crystal Palace 3-1.AFC Bournemouth na Sunderland 1-1 na Aston Villa na WBA.

C.RONALDO MARUFUKU KWENDA MOROCCO KUMTEMBELEA MSHIKAJI WAKE

C.Ronaldo amepigwa marufuku na Raisi wa Real Madrid F.Perez  kwenda Morocco kumtembelea rafiki yake Badr Hari.Perez amekwenda mbali anaweza kuomba wa Mfalme wa Morocco na rafiki Mohamed VI ili kumjulisha kama Ronaldo atakwenda huko.

Kitendo hicho cha C Ronaldo kwenda morocco kilishuhudia kiwango chake kushuka sana katika kipindi kifupi.

Cristiano Ronaldo and Badr Hari

ANGALIA HII-NICK CANNON AIBEZA KIAINA PETE YA UCHUMBA YA MARIAH CAREY

Need some TLC? Nick Cannon feigned heartsickness in a humorous snap with Kevin Hart's help before congratulating ex-wife Mariah Carey on her engagement to billionaire James Packer on Friday

Friday, January 22, 2016

TAREHE YA KURUDIA UCHAGUZI ZANZIBAR YAWEKWA WAZI

Habari za hivi punde tume ya uchaguzi chini ya Jecha imetangaza siku ramsi ya marudio ya uchaguzi mkuu Zanzibar kuwa ni Machi 20,2016.

Uchaguzi utahusisha:
1.Uchaguzi wa Raisi

2.Wajumbe wa baraza la wawakilishi

3.Madiwani

Hivyo katika kipindi hakutakuwa na uteule mpya wa wagombea wala kampeni.

Tokeo la picha la JECHA

KIINGEREZA BADO CHANGAMOTO KATIKA UFAULU

Lugha ya  kiingereza bado imekuwa mtihani mkubwa katika elimu ya Tanzania na hii inaweza kuonekana katika ngazi zote za elimu nchini Tanzania bado uelewa na ufaulu wake umekuwa mdogo sana.

Matokeo ya darasa la nne yametoka na soma ambalo wanafunzi wamefanya vibaya ni somo la Kiingereza ambapo ufaulu wake ni asimilia ndogo chini ya 60 ukilinganisha na masomo mengine yenye ufaulu wa zaidi ya asilimilia 80.

Tokeo la picha la primary students in tanzania 

BRT KITENDAWILI BADO WAKAZI WA DAR ES SALAAM WAISUBILIA HATMA YAKE KWA HAMU

Licha ya matokeo mengi kuhusu kuanza kufanya kazi kwa mradi wa mabasi yaendeyo kasi Dar es salaam ali maarufu BRT.Hamna wa kutengengua kitendawili ni lini mabasi haya yataanza kazi na kuwapa nafuu wakazi wa jiji la Dar es salaam.Awali ilikuwa katikati ya Desemba ikaja Januari 10.Tarehe zote hizo hakuna kilichotekelezwa huku ikiaminika sasa mradi unaweza chukua muda mrefu sasa.

Tokeo la picha la BRT PHOTO IN TANZANIAWakazi wa dar wakiangalia mradi

Tokeo la picha la BRT PHOTO IN TANZANIA

Labda ingeweza kupunguza adha hii kwa wakazi wa morogoro road kuacha magari yao

Thursday, January 21, 2016

Utafiti waonyesha ukosefu wa ajira kuongezeka ifikapo mwisho wa mwaka huu

Tatizo la ajira duniani linaweza ongezeka mwishoni mwa mwaka huu itafiti wa ILO umetabainisha hilo na inatarajiwa watu mil2.3 watapoteza ajira zao duniani kote na inaweza kuongezeka kwa makwa 2017 kufika mil 2.5.Sababu kubwa ni kudorora kwa uchumi na hivyo ubunifu wa ajira umepungua sana.Hili ni tishio hasa kwa nchi maskini ambao vijana wengi wamekuwa wakitegemea ajira za kuajiriwa ambazo zimekuwa zikipungua siku hadi siku kutokana na kukosa viongozi bora na serikali ambazo hazina utawala bora zikibujikwa na matumizi mabaya ya fedha za umma(rushwa.

Stock Photo - Man search job. Fotosearch - Search Stock Photography, Print Pictures, Images, and Photo Clip Art

Wednesday, January 20, 2016

Hali yaanza kuwa tete ndani ya siku zaidi 70 baada ya Raisi wa awamu ya tano kuapishwa

Tokeo la picha la magufuli
Hapa kazi tuu

Kumekuwa na vilio vya hapa na pale juu ya mwenendo mzima wa kipato cha mtu binafsi ndani ya nchi yetu katika kipindi hichi cha Raisi Magufuli huku wengi wakilalamika maisha ni magumu sana.Mara baada ya Raisi kuingia madarakani kipaombele chake kilikuwa ni kupunguza matumizi yasio ya lazima ndani ya serikali na badala yake fedha ziende kwenye matumizi yenye tija na kukusanya kodi.

Hatua hii ya serikali kutangaza vita hiyo inaonekana kuwa shuburi nzito katika maeneo mbali mbali kwa mfano,Baa ,Hoteli,Catering,Makampuni binafsi.Utafiti unaonyesha kuwa mapato yamepungua kwa kiasi kikubwa hasa na inaoneka hali hii inaweza kuwa tishio kwa ustawi ya sekta hizo.

Nini kinaweza tokea sasa upo uhakika kabisa baadhi ya waajiri kuamua kupunguza wafanyakazi na hivyo kuongeza tatizo la ajira ndani ya nchi.Hata wale ambao walikuwa wamejiari wanaweza kushindwa tena kwani kuna baadhi walitegemea semina na warsha za serikali ili wapate tenda.

Mimi binafsi naamini hali itakuwa sawa tuu hata kipindi cha Mkapa wananchi walipitia hali hii,ni ujinga kuendelea kutumbua hela za serikali na kunufaisha watu wachache kwa dili za semina na warsha zisijo na tija huku hali kwa mwananchi wa kawaida akikosa mahitaji muhimu.Magufuli aeendelee na kasi hii ili wananchi watambue heshima ya kufanya kazi zaidi kuliko kuamini katika njia za mkato zisizo na tija kwa taifa.

Hizo ni siku 70 tuu je ndani ya siku 1750 ya uongozi wake tutakimbia nchi?

Waziri wa Elimu afutilia mbali mfumo wa GPA.

Tokeo la picha la ndalichako

Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Mafuzno ya Ufundi ameamua kurejesha mfumo wa zamani wa Madaraja(Divion) badala wa uliokuwa unatumika sasa wa GPA.Hii imekuja baada ya kuwapa NECTA muda wa kupitia mfumo huo sasa na waje na sababu za kisayansi kwani mfumo huo unatumika

Waziri akitoa tamko alieleza baadhi ya mapungufu ya mfumo wa GPA 

1.Mgongano wa mkubwa katika kupanga GPA kuanzia sekondari mpaka vyuo vya ualimu

2.Ufinyu wa uelewa kwa watahiniwa kwani viwango vya kufaulu vimeshuka

3.Wadau hawakuhusishwa katika kuratibu mfumo huyo utumike,hata kamishina wa elimu hajatoa kibali.

Hivyo Prof J Ndalichako ameamua kurudisha mfumo wa zamani wa madaraja.Lakini serikali kupitia wizara hii inahitaji kurekebisha mambo mengi ya msingi katika elimu ambayo imekosa mvuto na kuanza kukosa mvuto.Mambo ni mengi sana ambayo yanapelekea kudorora kwa elimu kubwa ni sera mbovu za mawaziri wanaokalia kiti hiki wengi wanaongoza kisiasa na sio kiataaluma wakati research zinaweza fanyika lakini hamna wa kufuatilia.Hata hivyo mazingira ya elimu kwa upande wa walimu na wanafunzi na vitendea kazi bado nis shida ndio maana kuna hitajika nguvu ya ziada.Kama Waziri ameonyesha nia ya sayansi itumike katika kufanya maamuzi juu ya elimu kunaweza kuwa na tija tuwape muda watimize malengo yao.

Monday, January 18, 2016

BEI YA MAFUTA YAZIDI KUSHUKA HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU 2003

Bei ya mafuta imezidi kushuka zaidi katika kipindi hichi cha 2016 hii kwa takwimu inaonyesha ni anguko la kihistoria kutokea tangu 2003 ambapo ilishuka mpaka dola 27.67 kwa pipa.Waatalamu wa uchumi wanabashiri anguko linaweza kuwa kubwa hadi kufikia kati ya dola 28-24 kwa pipa hii inaweza kuwa kwani IRAN nchi inayotoa mafuta kwa wingi kwa sasa imefutiwa vikwazo vyake.Hivyo Iran  inaweza ongeza uzalishaji maradufu kwa mapipa nusu milioni kwa siku,nchi inashika nafasi ya 4 duniani katika utoaji wa mafuta.

Tokeo la picha la photos for oil extraction

Sunday, January 17, 2016

ROONEY APIGA GOLI LA MWAKA AIPA MAN U POINTI TATU

Wayne Rooney licha ya kusakamwa na vyombo vya habari hivi karibu leo ameonyesha kile ambacho mashabiki wa Man U walikikosa siku nyingi baada ya kufunga goli maridadi katika dk 78' dhidi ya Liverpool na kuipa timu yake pointi tatu muhimu na kufikisha alama 37 huku ikishika nafasi ya tano katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.Liverpool licha ya kutengeneza nafasi nzuri za ushindi walishindwa kabisa kuweka mpira kimiani huku De Gea akiwa katika kiwango chake aliweza kuokoa nafasi nzuri za Liverpool kupata goli hivyo Liverpool inaendelea kuwa na pointi 31 ,nafasi ya 9 katika ligi kuu ya Uingereza.

Manchester United striker Wayne RooneyRooney akifunga goli nzuri dhidi ya Liverpool.

ARSENAL BADO BADO SANAAA UBINGWA UINGEREZA

Timu ya Arsenal imeshindwa kujikita kileleni mwa Barclays Premier ligi leo kwa kushindwa kupata pointi zote tatu muhimu katika kipindi hichi baada ya kuambulia sare tasa dhidi ya Stoke City.Kwa matokeo hayo Arsenal licha ya kuongoza ligi kwa tofauti ya magoli dhidi ya leicester City,kama wataendelea kucheza kwa kiwango cha leo basi Ubingwa wa Uingereza utaendelea kuwa historia tena.

Arsenal inakosa kiongozi imara ndani ya timu anayeweza kubadilisha matokeo ndio maana wanaishia kupiga pasi ambazo hazina manufaa na mwisho wanakosa matokeo hari ya wachezaji kutaka ubingwa kwa Arsenal iko mbali sana.Inabidi Wenger atambue vipindi ambavyo timu inahitaji ushindi kitu ambacho kimeo adibu sana kwa arsenal tangu kipindi kile cha kina Thiery Henry,Patrick Viera,Dennis Be,Wiltod,Fred L,Robert P n.k.timu inacheza mechi zote kwa kiwango kile kile.Kwa matokeo hayo Arsena mpaka sasa ina alama 44 nyuma ya Leicester alama 44 na Man City 44.

Arsenal Stoke

Thursday, January 14, 2016

BAADA YA DAVID BOWIE KUFARIKI MUME WA CELINE DION NAYE AFARIKI

David Bowie mwanamuziki maarufu wa Rock aliyefariki wiki kwa ugonjwa wa Kansa akiwa na umri wa miaka 69.

Tokeo la picha la david bowie

Davis Bowie

Mume wa Celine Dion naye amefariki jana kwa ugonjwa wa kansa akiwa na miaka 73(Rene Angelil) ambaye wameishi nae kwa zaidi ya miaka 20 ni huzuni Mungu ametoa na ametwaa.

hhh
Rene enzi hizo na na Familia yake

Mohamed Elneny rasmi Arsenal Fc

Arsenal wamefanikiwa kumsajili kiungo mkabaji raia wa Misri Mohamed Elneny kwa ada ya uhamisho wa Pound 5m kutoka Balse ya Switzerland.Tayari tangu alhamisi ameanza mazoezi tayari kwa mechi za ligi kuu na championi ligi.Bado ndio kwanza ana umri wa miaka 23 hivyo atafanya makubwa kama ataweza kwenda na kasi ya ligi maarufu ya Barclays Premier Ligi.

Tokeo la picha la mohamed elneny

Wednesday, January 13, 2016

DR SHEIN ATOA MATUMAINI MAPYA SIKU YA MAPINDUZI YA MIAKA 52 JANA,SEIFU AKACHA

Tokeo la picha la dr shein

Hali ya siasa ya Zanzibar bado haiko sawa hasa baada ya Maalim Seifu Makamu wa Raisi kusema hatoweza kuhudhuria sherehe hizo.Dr Shein ambaye katiba bado inamtambua kama Raisi halali wa Zanzibar jana alitoa matumaini mapya baada ya kuwaeleza umma wa wananchi wa Zanzibar kuhusu mzozo wa kisiasa kuwa mpaka sasa hivi mazungumzo yako katika hatua nzuri na uchaguzi utafanyika tena kulingana na katiba inavyosema hivyo wananchi wanapaswa kusubili tarehe rasmi ya kupiga kura.

ARSENAL NA LIVERPOOL MTOTO HATUMWI DUKANI LEO USIKU CHELSEA MAN CITY WOTE UWANJANI,RATIBA YA MECHI NYINGINE HAPA

Liverpool manager Jurgen Klopp


Arsenal na Liverpool zinakutana leo katika mchezo wa ligi kuu,
timu zote zikiwa zinasummbuliwa na majeruhi wengi Arsenal itaendelea kumkosa Alexis naCarzola  na wengine na Liverpool inaweza kuwacheza wachezaji wake waliokuwa majeruhi Ibe,Jordan Henderson na Millner

Tokeo la picha la PREMIER LEAGUE LOGO

Mechi Nyingine 

Tuesday, January 12, 2016

MANCHESTER UNITED BADO KIMEO HUKU ASTON VILLA YAPATA USHINDI WA KWANZA.MATOKEO YOTE HAPA.

Paul Dummett rescues a point for NewcastleDiGea akiangalia goli la Newcastle

Manchester baada ya kupata ushindi wiki iliyopita katika FA cup jana gonjwa lake la kukosa ushindi limeendelea baada ya kupata sare ya 3-3 dhidi ya Newcastle United.Rooney akifunga mara mbilli 9' na 79 ' na Lingard 38' kabla ya Newcastle kujibu mapigo Wijnaldum 42  Mitrovic 67′ na Dummet 90'.

Aston Villa imepata ushindi wake wa pili katika Ligi kuu kupiitia kwa Lescott 58' ,Licha ya Bournemouth kuanza kushinda ilishuhudia ikipata kichapo kutoka kwa West Ham.


Friday, January 8, 2016

SERIKALI YATOA PICHA MAALUMU YA RAISI JOHN POMBE MAGUFULI KWA MATUMIZI YA OFISI BINAFSI NA SERIKALI

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maelezo na Habari Zamaradi Kawawa akiongea na waandishi wa Habari leo alionyesha picha rasmi ya Mh John Pombe Magufuli ambayo ndio itakayotumika katika ofisi zote za binafsi na serikali.Kwa maelezo ya Kaimu Mkurugenzi huyo picha hiyo itauzwa kwa gharama ya shs 15,000 tu bila Fremu.Pia alitoa onyo kwa wale wanjanja wa kucopy na kupaste kuwa picha hiyo itapatikana katika taasisi hiyo ambayo ndio inamaamlaka ya kuuza picha hiyo.

Dar es salaam.

Habari Maelezo Mtaa wa Samora.

Mikoani

Kwa wakala wa manunuzi serikali kwa mikoa yote. 


Zamaradi Kawawa.


Thursday, January 7, 2016

KAMA HUJUI SAMATTA NDIYE MCHEZAJI BORA AFRICA ABEBA TUZO JANA USIKU

Mchezaji wa kimataifa kutoka Tanzania Mbwana Ally Samatta amefanikiwa kuwa mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika.Hakika Samatta ameweza kuwa shujaa na mwanamapinduzi wa ukweli nje ya Tanzania haya ni mafanikio binafsi lakini kwa Taifa pia limepata faida kubwa.

Ni wakati sasa kwa wachezaji wengine kujiwekea malengo kuweza kuvuka record hii ya Samatta ambaye kwa habari za sasa anaacha na TP Mazembe ili kwenda Ulaya kama dili zake zitafanikiwa.Na hivyo anaweza kuja kukaa tena meza moja kugombea zawadi ya kuwa mchezaji bora nje ya Afrika kama tulivyo ona kina Toure,Etoo n.k.Na hakika kwa matazamo wa Samatta atafanikiwa.

12407463_1651933801734351_1469028646_n

SIMBA YAWAFUNGA WAKUSANYA MAPATO WA UGANDA(URA)

Simba jana usiku iliweka matumaini ya kusonga mbele zaidi katika mashindano ya Mapinduzi yanayofanyika Zanzibar baada ya kuifunga URA bao 1 bila na kukusanya pointi 4 mpaka sasa.

Ibrahim Ajib ndie aliyekuwa shujaa wa jana baada kufunga goli safi katika kipindi cha kwanza.Ajib alipiga shuti la mbali ambalo lilimshinda kipa wa URA.Kipa wa Simba nusura awazawadie URA goli baada ya kushika mpira aliorudidhiwa na kuwapa URA nafasi ambayo walishindwa kuitumia.Mpaka kipindi kinaisha Simba 1 URA 0.

Tokeo la picha la ajib ibrahim